I WISH U A MARRY XMASS & HAPPY NEW YEAR 2012

click the word video above 2 watch the clips & cloz 2 back

Monday, February 8

RAIS JAKAYA KIKWETE AOMBOLEZA KIFO CHA MNIKULU RAJABU MOHAMMED KIANDA



Mama Salma Kikwete akimfariji Bi.Khadija Kianda mjane wa Marehemu Rajabu Kianda aliyekuwa mnikulu kufuatia kifo chake kilichotokea jumapili jijini Dar es Salaam.

akitoa heshima za mwisho mbele ya jeneza la aliyekuwa mnikulu Bwana Rajabu Kianda aliyefariki jana jijini Dar es Salaam.Marehemu Kianda anatarajiwa kuzikwa leo (tarehe 9/2/2010) nyumbani kwao Kihurio Same Mkoa wa Kilimanjaro.


akimfariji Bi.Khadija Kianda ambaye ni mjane wa Marehemu Rajabu Kianda aliyekuwa Mnikulu ambaye alifariki dunia Jumapili jijini Dar es Salaam.Rais Kikwete alikwenda nyumbani kwa marehemu eneo la Mikocheni jijini Dar es Salaam kuifariji familia ya marehemu ambaye anatarajia kuzikwa huko Kihurio Same,Mkoani Kilimanjaro.Pembeni ni Mama wa Marehemu Bi. Mwanahawa Samuel.

MNYIKULU- Hili ni neno la kinyamwezi lilikokuwa likitumiwa wakati ule wa utawala wa kitemi, Mtemi Mirambo wa wanyamwezi alikuwa na wasaidizi wake, hawa walikuwa wakiitwa "Wanyikulu" kwani nyumba ya mtemi ilikuwa ikiitwa "IKULU" sehemu ambapo maamuzi ya vita na mipango yote ya kiutawala inafanyikia. Hivyo basi sisi wanyamwezi tulikuwa tunawaita wasaidizi wa mtemi kuwa ni "WANYIKULU" ambao walikuwa na dhamana ya kuhakikisha mambo yote ya kiutawala yanaenda kama kawaida wakisaidiwa na "MAKATIKILO"-hawa ni kama wajumbe wapeleka habari. hivyo mnikulu ni mtendaji mkuu ikulu ya rais.