I WISH U A MARRY XMASS & HAPPY NEW YEAR 2012

click the word video above 2 watch the clips & cloz 2 back

Thursday, November 25

Mwakyembe ashangaa kocha kumpanga ktkt ..amuuliza kocha nifunge wapi?..kocha akamjibu popote...

SIASA ni mchezo mgumu. Kama ilivyo katika kandanda, aliye nje anayaona makosa, mengi. Walio uwanjani wanaujua uchungu wa game.

Jana nimemwona JK akitangaza baraza lake, si JK wa siku zote. Alikunja uso mara kwa mara. Kuna aliowakunjia uso. Wanasema; kumkoma nyani giladi. Ukitaka kumwua nyani usimtazame usoni.

Sura mpya zilikuwa nyingi. Majina mapya. Kuna majina aliyataja huku akionyesha kuwa anaowataja si watu wake wa karibu. Hakukuwa na ’ mtani wangu nanihii!’

Kama kocha, kikosi kile kinaweza kufanya maajabu. Chaweza kuwa kikosi cha kujituma, maana, wengi waliongizwa kikosini ni wapya. Wanajua nje kwenye benchi kuna wapya wengine, kuna wazoefu. Wakiboronga mchezo, kuna watazamaji watakaopiga kelele majukwaani; ” JK mwingize nanihii!, Mwingize nanihii!”. Ndio mchezo wa siasa ulivyo, kama kandanda vile, kocha ana kazi ngumu, na walio uwanjani pia.

Habari kubwa jana; Samwel Sitta na Harrison Mwakyembe. Kwanini JK amemchezesha Harry Mwakyembe katikati pamoja na akina Jo’ Magufuli na Anna Tibaijuka? Huenda hata Mwakyembe mwenyewe ameshangaa kocha kumpanga katikati. Na labda ameuliza; ” Kocha nifunge wapi?”

JK atamjibu; ” Funga Kote Kote! Anampima akili yake? Na Kwanini Sam Sitta katupwa wingi ya kulia? Nahofia, Sitta ataisubiri sana mipira. Mingi itaishia katikati, hataipata! Ni lazima afanye jitihada binafsi kuitafuta mipira. Na kuna watazamaji jukwaani wanaofikiri, kuwa ingekuwa busara Sam Sitta angechagua kukaa kwenye benchi kulinda heshima yake.
Wanaosema hivyo hawaujui ugumu wa mchezo wa siasa. Sitta atalazimika Ku- ’Like The Situation’ - Kuipenda Hali, basi. Masikini Samwel Sitta, si huyu aliyekuwa na mhimili wake wa dola aliokuwa akiuongoza.

Na ni Sitta huyu huyu aliyepata kutamka bungeni; ” Wapinzani mtaitwa hivyo hivyo, wapinzani, maana nyie mnapinga-pinga tu!”. Alimjibu aliyekuwa Kiongozi wa upinzani Bungeni Hamad Rashid aliyesema kuwa wakati umefika kwa kambi ya Upinzani kuitwa ’ Kambi ya Ushindani’ ili kuondoa dhana ya upinzani ambayo jamii inaitafsiri vibaya.

Masikini Sitta, akiwa Spika wa Bunge alikuwa na nafasi ya kuacha legacy ya kuwezesha hoja ya Watanzania kupata Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi ijadiliwe bungeni. Ndio, Samwel Sitta sasa atakumbukwa pia kwa kuwa Spika wa kwanza kujenga ofisi yake ya Spika kwao Urambo Mashariki. Ofisi yenye thamani ya mamilioni ya fedha za walipa kodi. Hivi alidhani Uspika ni Usultani?!

Naam. Na kwenye mchezo mgumu wa siasa kuna kinachoitwa ’ Inner cabinet’. Kikundi kidogo cha mawaziri kinachoweza kukutana na Rais hata isipo rasmi. Kitapanga mikakati kabla ya kukutana na baraza zima. Kama kuna ’ Inner Cainet’ pale Magogoni, basi, sina hakika kama Sam Sitta na Harry Mwakyembe watakuwamo. Si ni juzi tu walikuwa ’ a political loose cannons’ ndani ya chama- Mizinga inayoning’inia, inapiga Kote Kote! Na bado ndani ya chama kuna hofu ya uwepo wa masalia ya ’ Weapons Of Mass Political Destructions’. Anne Kilango, Ole Sendeka.....

Naam. Katika miaka ya karibuni, inaaminika kuwa Bungeni Sitta aliipa tabu sana Serikali. Bado hatujaandika, na itakuja, simulizi ya ’ Mitume 12’ iliyopambana na ufisadi ndani na nje ya bunge. Samwel Sitta alikuwa mmoja wa mitume hiyo. Harry Mwakyembe nae alikuwamo. Hawakujua kuwa, ni kazi ngumu sana kupambana na ufisadi kwa kelele za bungeni tu. Dawa ni Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi. Ndio, tatizo ni MFUMO uliopo ambao nao walikuwa ni sehemu ya mfumo huo.
Katika mchezo wa siasa; adui yako usimwache nje ya hema akunanilihii haja ndogo ukiwa ndani ya hema. Mwingize ndani ya hema ananilihii haja ndogo nje akiwa ndani ya hema.

Naam.Wanaosema siasa ni mchezo mchafu wanakosea. Siasa ni mchezo mgumu, basi.

Na Maggid, Iringa Novemba 25, 2010

Wednesday, November 24

HapPy B.dAy Jokha RaShiD

Jokha Rashid
Leo ni siku ya kuzaliwa Jokha Rashidi 25.11....Blog hii na kwa niaba ya ma class mate wake wote waliosoma nae Mkwakwani sec sch Tunamtakia furaha yeye na familia yake yte,Mmungu ampe afya njema ktk maisha yke na mafanikio ktk siku zake nyingine za usoni.

We wish u happy b.day

BARAZA JIPYA LA MAWAZIRI TANZANIA


1. Ofisi ya Rais (Utawala Bora) Mathias Chikawe

Ofisi ya Rais – Mahusiano na Uratibu: Stephen Wassira

2.Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma Hawa Ghasia

3. Ofisi ya Makamu wa Rais – ( Muungano) Samia Suluhu

2. Ofisi ya Makamu wa Rais – (Mazingira) Dr. Terezya Luoga Hovisa

4. Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge): William Lukuvi

2. Uwekezaji na Uwezeshaji Dr. Mary Nagu

5. Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) George Huruma Mkuchika

Naibu: Aggrey Mwanri

Naibu: Kassim Majaliwa

6. Wizara ya Fedha Mustapha Mkulo

Naibu: Gregory Teu

NAibu: Pereira Ame Silima

7. Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Shamsi Vuai Nahodha

Naibu: Balozi Khamis Suedi Kagasheki

8. Wizara ya Katiba na Sheria Celina Kombani

9. Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard K. Membe Naibu: Mahadhi Juma Mahadhi

10. Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dr. Hussein Ali Hassan Mwinyi

11. Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Dr. Mathayo David Mathayo

Naibu: Benedict Ole Nangoro

12. Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Prof. Makame Mnyaa Mbarawa

Naibu: Charles Kitwanga

13. Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Prof. Anna Tibaijuka Naibu: Goodluck Ole Madeye

14. Wizara ya Maliasili na Utalii Ezekiel Maige

15. Wizara ya Nishati na Madini William Mganga Ngeleja 1. Adam Kigoma Malima

16. Wizara ya Ujenzi Dr. John Pombe Magufuli

Naibu: Dr. Harrison Mwakyembe

17. Wizara ya Uchukuzi Omari Nundu

Naibu: Athumani Mfutakamba

18. Wizara ya Viwanda na Biashara Dr. Cyril Chami

Naibu: Lazaro Nyalandu

19. Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dr. Shukuru Kawambwa

Naibu: Philipo Mulugo

20. Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dr. Haji Hussein Mpanda

Naibu: Dr. Lucy Nkya

21. Wizara ya Kazi na Ajira Gaudensia Kabaka Makongoro Mahanga

22. Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Sophia Simba Umi Ali Mwalimu

23. Wizara ya Habari, Vijana na Michezo Emmanuel John Nchimbi

Naibu:Dr. Fenella Mukangara

24. Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki Samuel John Sitta

Naibu Dr. Abdallah Juma Abdallah

25. Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika Prof. Jumanne Maghembe

Naibu: Christopher Chiza

26. Wizara ya Maji: Prof. Mark James Mwandosya

Naibu: Eng. Gerson Lwinge

Monday, November 22

HaPpY biRtHdAy Sadallah Mbeyu


Leo ni siku ya kusherehekea siku ya kuzaliwa kwa aliyekuwa Makamu Mkiti mstahafu 2008/9 wa jumuiya ya wanafunzi wa kitanzania waishio mjini Hyderabad (TSAH),Mimi M/kiti mstahafu Nkya 2009/10 na kwa niaba ya vijana wa Tolichowki na watz wote hapa hyderabad tunapenda kumtakia kila la kheri na mafaniko ktk maisha yake ya usoni Mmungu akuzidishie umri ktk maisha yako



Sunday, November 21

ChaSin money...MoNEy...

TAMKO LA VIJANA WASOMI WA VYUO VIKUU WA MKOA WA DODOMA, KUHUSU KITENDO CHA BAADHI YA WABUNGE WA CHADEMA KUTOKA NJE YA UKUMBI WA BUNGE.


NDUGU WAANDISHI WA HABARI, NDUGU WANANCHI,.
wali ya yote nawashukuru sana kuhitikia wito wetu wa gfafla kuja kujumika pamoja nasi leo hii, akhsanteni sana.

Sisi vijana wasomi wa vyuo vikuu mbalimbali vilivyoko mkoa wa Dodoma kwa pamoja tunapenda kuweka wazi maoni yetu juu ya kitendo kilichofanywa na Wabunge wa CHADEMA jana 18.11.2010 wakati Mhe. Rais alihutubia Bunge.

Kwanza tumeshtushwa na kitendo hicho na kuweka wazi masikitiko yetu kwa kuwa kilichofanyika ni kinyume na matarajio ya wapiga kura waliowachagua waheshimiwa wabunge hao kuwawakilisha ndani ya chombo hicho kikubwa na chenye heshima kubwa ndani na nje ya nchi.

Bunge ni sehemu ya kuwakilisha wananchi kwa hoja chini ya kanuni zilizopo bila kujali itikadi ya chama chochote cha siasa na kazi kubwa ya mbunge ni kuishauri na kuisimamia Serikali kwa niaba ya wananchi waliomchagua au kuwachagua.

Kwa mantiki hiyo basi kama Wabunge hawamtambui Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania maana yake hawana kazi ya kufanya ndani ya Bunge kwani kazi yao kubwa ni kuishauri na kuisimania Serikali sasa kama hawaitambui Serikali hiyo hawana sababu ya kuendelea kuwepo Bungeni.

Pili Baada ya uchaguzi wa Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda, wabunge hao pia walinukuliwa na vyombo vya habari na ushaidi tunao wakiweka wazi kumkubali kiongozi huyo, na kauli mbiu yake ya ‘Bunge moja’ je, kitendo walichofanya inaashiria utekelezaji wa kauli mbiu ya Bunge moja?

Tatu msimamo wa kutomtambua Rais ni wa CHADEMA kama chama na waliotoka nje ya Bunge ni wabunge sasa ni vema wabune hao watambue na kutafakari upya kama kweli wanawawakilisha Bungeni wananchi au cha na kutekeleza misimamo yao bila kujali maslahi ya waliowachagua na kumpa kura nyingi Rais Kikwete?.

Nne Kwa badhi ya wabunge wa CHADEMA kutomtambua Rais wakati akilihutubia bunge ni wazi kuwa hata sheria zitakzopitishwa na Bunge hawatahusika kwa kuwa mwenye mamlaka ya mwisho kukubali sheria iliyotungwa na Bunge itumike ni Rais ambaye wanadai hawamtutambui.
Ni dhahiri kuwa watashindwa kufanya kazi yao ya uwakilishi na usimamizi wa Serikali Bungeni .

Je wanawaonesha watanzania dalili gani kama si kutaka kuleta machafuko nchini na mgawanyiko ndani ya Bunge na kwa Jamii kwa ujumla?.

Wananchi waliowachagua wabunge hao wanapaswa kutafakari upya wawakilishi waliowachagua kama wana uelewa wa kutosha kuhusu bunge, sisi vijana wa vyuo vikuu tunajua na tunatambua kuwa Rais ni Sehemu ya Bunge na Bunge haliwezi kukamilika bila Rais na hii ndio maana kila sheria inayopitishwa na Bunge ni lazima yeye Rais aweke sahihi yake.

Katika mazungumo yake na waandishi wa habari wiki hii Mweneykiti wa CHADEMA MHE. Freeman Mbowe, alinukuliwa na vyombo vya habari akisema wabunge wake na madiwani wanaweza kuendelea kuwakilisha wananchi licha ya kutomtambua Rais.

Sisi tunasema hili si sahihi bali ni upotoshaji mkubwa, kamwe mtoto hawezi kudai kuwa hamtabui Baba yake kisha anaendelea kumwita Baba na kutumia kila kitu kinachotolewa na Baba huyo huyo. Huo ni utovu wa nidhamu au kukosa maadili.

Sisi vijana wa vyuo vikuu Mkoa wa Dodoma tunawaomba Watanzania wote wenye nia njema na Taifa letu kuwapuuza wabunge wa CHADEMA na kutambua kuwa lengo lao ni kutaka kutuhamisha kutoka kwenye ajenda ya msingi ya Maendeleo na kubaki kwenye malumbano ya kisiasa kama tulivyoshuhudia katika nchi jirani.

Kamwe tusikubali kudanganywa na watu wachache.

Mwisho tungependa kuwaomba Wabunge wa CHADEMA wawaombe radhi watanzania kwa kuvuruga tashwira safi ya Bunge letu lisilo na ubaguzi na itikadi za kisiasa vinginevyo wanawadharau watanzania waliowachagua wakidhani kwamba niwaadilifu wa Taifa na si cha chama chao.

Tutambue kuwa kazi kubwa ya CHADEMA na Wabunge wake kwa sasa ni kuwachanganya watanzania ili badala ya kuendelea na shughuli za ujenzi wa taifa wabaki na malumbano ya hapa na pale kwa manufaa yao binafsi.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Bunge letu na kutuepusha na ubaguzi kama huu uliofanywa na baadhi ya Wabunge wa CHADEMA.
Aksanteni sana.

IMESOMWA NA THOBIAS MWESIGA RICHARD
KWA NIABA YA WANAFUNZI WA VYUO VIKUU MKOA WA DODOMA

Saturday, November 20

this was the tru teacher ...

Mapenzi ni afya, ni kila kitu lakini yana kanuni zake!


Haihitaji papara kuamua kuhusu mwenzi wa maisha yako. Kuna fahari ya macho na kinachogusa mtima. Usimuone barabarani ni mzuri, ukakurupuka. Unatakiwa ujadiliane na moyo wako halafu mpate jibu linalokubalika. Kupata mwenzi wa maisha ni sawa na Serikali ya Umoja wa Kitaifa. Tofauti na ile ya Zanzibar au Kenya, hii inahusisha maridhiano kati ya macho na moyo. Macho yanaona na kuvutiwa, moyo unaguswa. Kwa mantiki hiyo, ni kosa kujiaminisha kwamba unapenda ikiwa moyo wako haujakubali. Lakini haiwezekani moyo ukapenda ikiwa macho yamekataa. Macho yanaona, ubongo unatafsiri halafu moyo unapokea. Umemkubali kwa jinsi alivyo, hapo ni sawa. Lakini unatakiwa kujiuliza maswali mengine 50 kuhusu yeye, halafu upate majibu ambayo yanaridhiwa na kila upande. Usifanye chaguo ambalo litaufanya moyo wako usinyae. ONYO: Kamwe usiruhusu moyo wako usinyae kwa sababu hiyo ni sawa na ugonjwa hatari. Moyo unaposhindwa kufanya kazi yake barabara, hutema sumu ndani kwa ndani ambayo inaweza kukusababishia matatizo makubwa nap engine kukua haraka. Kuwa makini. Maswali ya kujiuliza ni haya; KABISA NIMEMRIDHIA? Hapa kuna maana kuwa tayari umemkubali lakini jiulize tena na tena kuhusu yeye. Kama kuna shaka ndani yake usilazimishe, badala yake pitisha uamuzi mmoja pale ambapo umeona majibu yanakuja chanya kila ulipojiuliza. NIPO TAYARI? Binadamu hajakamilika, pengine kuna mambo yanayomzunguka mwenzi wako. Watu wa pembeni wanazungumza, lakini pia si ajabu ikawa kuna vikwazo vya kifamilia. Swali hili linachukua nafasi katika eneo hilo. Jiulize kama upo tayari kukabiliana na presha za watu na ndugu ilimradi uhakikishe unambakiza kwenye himaya yako. Isitokee ukasema upo tayari leo lakini baada ya muda ukamfanya mwenzako ajute. Jiridhishe leo kwa faida ya maisha yenu kwa jumla. U-tayari wako uwe na maana kuwa hata miaka 10 ijayo, utamtetea popote kwamba ulilolisimamia leo, utaendelea nalo kila siku mpaka Mungu atakapoamua kutumia mamlaka yake kuwatenganisha. SITAMCHOKA? Usithubutu kupenda kwa fahari ya jicho la leo. Nimekutaka ujadiliane na moyo wako kwa sababu kuna vitu vingi vya kujiridhisha kabla ya kuamua kuzama moja kwa moja. Ikiwa kuna dalili kwamba ipo siku utamchoka usithubutu kumpotezea muda. Mwenzi wa maisha ina maana ni mtu wa furaha yako kwa maisha yako yote. Kwamba yeye atakuwa sehemu ya maisha yako. Hivyo, huyo hatakiwi kuchokwa bali anastahili hifadhi ya kudumu moyoni kuliko mwingine. Mtu ambaye unaweza kumchoka mbele ya safari utamjua tu kwa kujiuliza. Ikiwa kuna penzi la kweli, hakika utaona ni kiasi gani linavyomea. Hutakuwa na shaka ya aina yoyote juu yake na utakubali kwamba furaha anayokupa leo, haitabadilika. Kuna penzi la usanii, kama hilo ndilo linalokuongoza basi ni vema ujitenge. Nina maana kuwa endapo humpendi kutoka moyoni ila unamdanganya, jitenge haraka kwa sababu mbele utamchoka, utamsumbua na utamsaliti. VIPI MAUDHI YAKE? Mpenzi wako ni binadamu siyo malaika. Hivyo ndivyo na wewe ulivyo. Nyoye ni viumbe dhaifu, kwahiyo kila mmoja ana upungufu wake lakini kwako ni vizuri ukajiuliza endapo maudhi yake unaweza kuyavumilia. Ni kosa kubwa kufukia mashimo kwa yale yanayokukwaza kwa mwenzi wako. Amua leo, ikiwa unaona kila kitu kinawezeka, kwamba pamoja na kasoro zake lakini anavumilika na upo tayari kufanya naye maisha, basi nenda mbele zaidi. Ruhusu moyo wako uamue katika maudhi yanayokusumbua kutoka kwa mwenzi wako. Moyo wako upime kwamba ubora wake upo juu kuliko kasoro zinazokutibua. Hapo unangoja nini tena? Mng’ang’anie huyo huyo, ukitaka asiye na kasoro utasubiri sana. NAWEZA KUONGOZANA NAYE? Hili siyo swali la kudharau hata kidogo. Kuna watu wengi wapo kwenye ndoa lakini hata siku moja huwezi kuona wameongozana na wenzi wao. Kuna vitu vingi vinawasibu, angalia nawe yasije yakakukuta kwenye safari yako. Akuridhishe kwa muonekano wake, kwahiyo uwe na imani kuwa hata ukiongozana naye barabarani utakuwa ni mwenye kujiamini. Hapa kuna la kujifunza zaidi. Hakuna maana kuwa utashindwa kuongozana naye kwa sababu ni mbaya, la hasha! Inawezekana mwenzi wako ni mzuri sana, kwahiyo mkiongozana watu huwashangaa. Pia, mwenzi wako anaweza kuwa na umbo kubwa, mnene, hivyo macho ya watu barabarani yanaweza kukufanya ukajiona mnyonge.

Thursday, November 18

PINDA ALA KIAPO


WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA AKILA KIAPO KATIKA IKULU NDOGO YA CHAMWINO DODOMA LEO. JK AKIMPONGEZA WAZIRI MKUU MARA BAADA YA KUMWAPISHA JK KATIKA PICHA YA PAMOJA NA WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA, RAIS MSTAAFU ALHAJ ALI HASSAN MWINYI, MAKAMU WA RAIS DK. MOHAMED GHALIB BILAL NA MAWAZIRI WAKUU WALIOSTAAFU MARA BAADA YA KUAPISHWA WAZIRI MKUU PINDA. VIONGOZI WAKUU WA SERIKALI YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA NA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR WAKIONGEA MARA BAADA YA KUAPISHWA WAZIRI MKUU PINDA. LEO JIONI JK ATAHUTUBIA BUNGE NA KULIZINDUA RASMI

Sunday, November 14

Monday, November 1

BREAKING NYUUUUUZZZZZZZ: DK. ALI MOHAMED SHEIN ASHINDA UCHAGUZI ZANZIBAR


Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar Bw. Khatib Mwinyichande akitangaza matokeo ya urais Zanzibar katika hoteli ya Bwawani mjini Unguja usiku huu
Rais mteule wa Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein akitoa
shukrani baada ya kutangazwa mshindi

Mgombea urais wa Chama cha Wananchi CUF
Maalim Seif Shariff Hamad akikubali matokeo

MGOMBEA WA CCM KATIKA KUGOMBEA URAIS WA ZANZIBAR DK. ALI MOHAMED SHEIN AMESHINDA URAIS ZANZIBAR KWA MUJIBU WA MATOKEO YA TUME YA UCHAGUZI SASA HIVI KWA ASILIMIA 66.4%

MAALIM SEIF SHARIFF HAMAD AKUBALI MATOKEO NA KUIPONGEZA CCM NA MGOMBEA WAKE. ANAHUTUBIA HIVI SASA NA KUMKUBALI DK. ALI MOHAMED SHEIN KWA KUPATA RIDHAA YA WAZANZIBARI KUWAONGOZA KWA MIAKA 5 IJAYO AKIWA RAIS WA AWAMU YA SABA VISIWANI HUMO.

HATA HIVYO MAALIM SEIF AMESEMA KUNA DOSARI ZINAZOTOKANA NA BADHI YA MAOFISA NA KUMUOMBA RAIS MTEULE KUWA MWANGALIFU NA HILO ILI NCHI ISIFIKE PABAYA.

AMESEMA KATIKA UCHAGUZI HUU HAKUNA MSHINDI AMA MSHINDWA. MSHINDI NI MZANZIBARI. NA KAMUOMBA RAIS MTEULE AHAKIKISHE HILO ILI HALI YA HEWA ISIJE KUCHAFUKA. ANAMALIZA HOTUBA NA KWENDA KUMPA MKONO DK. SHEIN HUKU VIFIJO NA NDEREMO VIKIUMUKA KATIKA KILE KILICHOITWA MATUMAINI MAPYA KWA ZANZIBAR.

DK. SHEIN ANAITWA KUONGEA SASA.ANAINUKA NA KUELEKEA KWENYE KIPAZA SAUTI. UKUMBI UMEJAA MSISIMKO SI WA KAWAIDA. ANAMFAGILIA MAALIM SEIF KWA HOTUBA FUPI LAKINI NZITO, ANAAHIDI KUSIMAMIA VYEMA UUNDAJI NA UENDESHAJI WA SERIKALI YA MSETO NA KUKUBALIANA NA MAALIM SEIF KUWA HAKUNA MSHINDI ILA WAZANZIBARI WOTE KWA MUSTAKABALI WA MAENDELEO YA VISIWANI.

GLOBU YA JAMII INAMPONGEZA
DK. MOHAMED ALI SHEIN KWA USHINDI HUU WA KIHISTORIA.

VIDEO YA TUKIO HILI INAANDALIWA. TUVUTE SUBIRA........
TUKIO HILI LINARUSHWA LIVE NA TBC ONE