I WISH U A MARRY XMASS & HAPPY NEW YEAR 2012

click the word video above 2 watch the clips & cloz 2 back

Monday, August 30

TANZANIA YACHUKUA KIKOMBE CHA MASHINDANO YA RAMADHANI MJINI HYDERABAD KILICHOANDALIWA NA JUMUIYA YA WANAFUNZI F.S.A INDIA 2010

Mashindano haya yanaandaliwa na jumuiya ya wanafunzi wa kigeni mjini Hyderabad kila mwaka ifakapo mwezi wa kiislam ramadhani.Mwaka huu jumuiya ya wanafunzi wa kitanzania (T.S.A.H) mjini hyderabad india waliingiza timu yao,katika kinyang'anyiro cha kombe hili la mwezi huu wa ramadhani.Ambapo timu ya Tanzania iliibuka kuwa mshindi baada ya kuizaba timu ya ELTREA 1-0.Hivyo kuibuka mshindi ktk kinyang'ang'anyiro cha kombe hili
Hawa ni wachezaji wa timu ya tanzania wakishangilia baada ya kupewa kikombe hichi,ktk mechi ya kwanza tanzania ilicheza na timu ya cameron ikashinda 4-3 ambayo yalikuwa ni magoli ya penati,na ktk mechi ya pili ilitoka Tanz 2-1 Sudan ,mechi ya tatu Tanz 3-1 AFGHANSTAN hivyo baada ya kuizaba timu hizo ndipo fainali walipokuja kuizaba tena ELTREA 1-0
KWA KWELI ILIKUWA PATA SHIKA NGUO KUCHANIKA MASHABIKI PAMOJA NA WACHEZAJI WALISHANGILIA SANA ..KWANI TOKA MASHINDANO HAYA YA RAMADHANI YAANZISHWE TZ HAIJAWAHI KUCHUKUWA KIKOMBE HICHI HII NI MARA YAKE YA KWANZA JAMANI TANZANIA TUKO JUUUUUUUUUUUUU
WATZ WAKISHANGILIA PIA KWA KUPEPERUSHA BENDERA YAO YA TAIFA KUONESHA UALENDO WAO WALIJIWEKEZA KTK NCHI YAO
KULIA KWAKO NI M/KITI WA JUMUIYA YA WANAFUNZI HYDERABAD INDIA ALIPATA PIC MOJA YA UKUMBUSHO NA TIMU YA TANZANIA
HUYU NI MAKAMU M/KITI WA JUMUIYA YA WANAFUNZI HYDERABAD LKN PIA NI MCHEZANI WA TIMU YA TZ HAPA AKIPONGEZWA NA MGENI RASMI BAADA YA KUIPATIA TIMU YKE USHINDI
Mchezaji wa kitanzania Bw Foba akipongozwa na mgeni kwa kazi nzuri walioifanya ..baada ya kuipatia yimu yao ushindi
Hizi ni baadhi ya jezi ambazo timu yetu iliwezwa kuzawadiwa baada ya kupata ushindi huu
Hapa watanzania wakishereheke ushindi wao
baadhi ya watanzania waliojitokeza kuangalia mpambano
Mwenye fulana nyeusi ni M/kiti wa jumuiya akiwa pamoja na wenyeviti wa nchi mbalimbali hapa mjini Hyderabad
kinadada wa kitanzania pia hawakuwa nyuma kushangilia ushindi wao
hapa wachezaji wa kitanzania wakipokea medali zao a ushindi

watz kazi nzuri sana ...
Mkiti wa kamati ya starehe Dani msemo akibusu kikombe kuonesha ishara ya ushindi tulioupata ..kijana..na hizi pics hapa ni mchakato wa huyu mheshimiwa kazi nzuri kijana mchakato mzuri
Mkiti wa jumuiya Bw Abdillah akiwa na wanajumiya kushangilia ushindi uliopatikana

HUYU NDIE MCHEAJI ALIYETUZABIA BAO LA USHINDI Bw Said Mihala hapa akipewa medani ya ushindi..kazi nzuri kijana unastahili zawadi
KWA KWELI WATZ WALIFURAHI SANA
KINADADA WA KITANZANIA WAKISHANGILIA USHINDI
HAPA ILIKUWA KABLA YA KUPEWA KIKOMBE CHAO ...WALIKUWA WAKISUBIRI KWA HAMU SANA
M/kiti wa jumuiya Bw Abdillah nkya akiwa na kipa wa tanzania Bw RAHIMU pamoja na Bw SHAKIR Wakiashiria tuko pamoja
Huyu ndie meneja wa timu ya tz hapa mjini hyderabad Bw enock akijimwagia maji baada ya kumaliza mechi
HAWA NI VIJANA WANAOKAA KARIBU NA UWANJA WA MASAB TANK ULIOCHEZEWA MECHI HII HAPA HYDERABAD WAAKAA KITONGOJI CHA TOLICHOKI WALISEREBUKA KUPITA KIASI
KWA KWELI WATZ WALIJITOKEZA KWA WINGI KUJA KUANGALIA MPAMBANO HUU HAPA MJINI HYDRABDA UWANJA WA MASAB TANK
kijana Dani msemo akionesha uzalendo na nchi yake yatanzania baada kuipeperusha bendera ya tz uwanja mzima
siku hii watz walipiga sana mavuvuzela
kwa kweli watz waliserebuka vya kutosha ktk kusherehekea ushindi huu...yaani kulichezwa bolingo la kufa mtu............

Thursday, August 5

matokeo ya kura za maoni kinondoni, kawe, ubungo na A-Taun leo


Jimbo la Kinondoni

Iddi Mohamed Azzan ameibuka kidedea baada ya kupata kura 6196, akifuatiwa na Mustafa Muro kura 3059 huku Shy-Rose Banji akipata kura 2830.

Wagombea wengine katika Jimbo hilo ni pamoja na;

Mpoki Mwambulukutu..... kura 985
Godwin Kabisa..... kura 443
Kakolwa Mbano..... kura 395
Nkuruma Munjori..... kura198
Mackdonald Lunyilija..... kura146
Issa Omari.....kura 111
Bakari Maige..... kura 98.

Jimbo la Kawe.

Katika jimbo hili Mwenyekiti wa Wazazi Wilaya ya Kinondoni Angela Charles Kizigha ameshinda kwa kupata kura 3140 akifuatiwa na Kippy Warioba aliyepata kura 2752 wakati Zainuddin Adamjee amepata kura 2466.

Wengine katika jimbo hilo ni;

Aric Suma..... kura 1576
Jumaa Pijei..... kura 646
Mohamoud Madenge..... kura 588
Margaret Lema..... kura 443
Dr Malima Bundara..... kura 340
Faustin Kikova..... kura 240
Omary Wahure..... kura 214
Dr Petrnilla Ngiloi..... kura 191
Harold Maruma..... kura 172
Biton Mwenisongole..... kura 160
Elias Nawera..... kura 140
Japhet Robi..... kura 78
Nicodumus Chegula..... kura 68.

Jimbo la Ubungo

Hawa Mgonja Ng'umbi ndiye anayeng'ara katika matokeo ya uchaguzi wa kura za jimbo hilo ambapo amepata kura 7970, akifuatiwa na Waziri wa Maliasili na Utalii Shamsa Mwangunga aliyeambulia kura 6998 wakati Nape Nnauye akiondoka na kura 3734.

Matokeo ya wagombea wengine katika jimbo hilo;
Alfred Nchimbi..... kura 848
Michael Lupiana..... kura 516
Perpetua Haule..... kura 393
Dr Apollo Kissai..... kura 316
Peter Msuya..... kura 216
Assumpta Nalitoleta....192
Gaspar Hizza..... kura 181
Eliona Nkya..... kura 159
Slaus Mwisomba..... kura 158
Zangina Zangina..... kura 107.
ARUSHA

Naye Woinde Shizza wa Globu ya Jamii Arusha anaripoti kwamba matokeo ya kura za maoni kwa upande wa ubunge jimbo la arusha Dk. Batlida Burian amepatakura 9970 na aliyekuwa mbunge wa miaka 5 iliyopita Mh. Felix Mrema amepata kura 4347, Dk. Hamis Said Kibola amepata kura 834, Deogratias Mtuo amepata kura 268, Aloyce Peter Kilimbo amepata kura 116, Michael Sekajingo amepata kura 105. Hivyo mshindi ni Dk. Burian

Kwa uapnde wa ubunge jimbo la aAumeru Magharibi Bw. Goodluck Joseph ole Medeye ameibuka mashindi na kummwaga aliyekuwa mbunge wa miaka 5 E Mh. Elisa Mollel na wengineo walioshinda ni Jeremiah Sumari katika jimbo lake la Meru.

TAHADHARI NONDOOOZ ZA CHUMA KIMOJA.

Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania
Tahadhari Kuhusu Ongezeko la
Vyuo Vikuu Batili (Degree Mills)

Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) imepewa mamlaka ya kisheria kuthibiti na kusimamia ubora wa viwango vya elimu na mifumo inayotumiwa na vyuo vikuu katika kukidhi viwango vya ubora wa elimu ya juu, kusimamia uthibiti na kuhakiki uhalali na viwango vya kitaaluma vya tuzo za digrii na stashahada zinazotolewa na taasisi za elimu ya juu ndani na nje ya nchi.

Ifahamike kwamba, tuzo hizo zinahusisha pia digrii za heshima ambazo vyuo vikuu vimepewa mamlaka ya kuwatunuku watu ambao chuo husika kimeona ama mtarajiwa kupewa digrii hiyo ametoa mchango mkubwa wa kitaalam katika eneo lake la kitaaluma, au ametoa mchango mkubwa katika masuala ya kuhudumia ustawi wa jamii. Utoaji wa tuzo za aina hii kwa kawaida ni uamuzi wa vyuo husika kwa kutumia mifumo yao iliyowekwa kisheria inayotoa mamlaka kwa chuo kufanya hivyo.

Kwa mantiki hiyo, Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania inatambua na kukubali uhalali wa digrii za heshima zilizotolewa na vyuo vikuu vilivyothibitishwa na vinavyotambuliwa na serikali au taasisi zilizokasimishwa mamlaka ya kufanya hivyo kwa mujibu wa sheria. Hata hivyo, digrii za heshima haziwezi kutumika kama sifa ya kitaaluma, kwenye jina la mhusika au vinginevyo, katika kutafuta ajira, kupandishwa cheo, au kama msingi wa kujiendeleza kielimu.

Katika miaka ya hivi karibuni Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania imebaini ongezeko la tuzo za digrii za uzamivu za heshima, yaani “honorary doctorates (honaris causa)” zikitolewa kwa watu wenye haiba na wadhifa mkubwa katika maeneo mengi ya Afrika. Hali hii pia inaongezeka kujitokeza kwa kasi nchini Tanzania. Haishangazi kuona kwamba katika kipindi cha muongo mmoja uliopita na hadi sasa hivi, watu maarufu wamekuwa wakitunukiwa digrii za aina hii kutoka katika taasisi ambazo kutambuliwa kwake kunatia shaka siyo nchini Tanzania tu, bali hata katika nchi zilimo taasisi hizo.

Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania inastushwa sana na suala hili la ongezeko na nyendo za taasisi na vyuo vikuu visivyotambuliwa nchini Tanzania na kwingineko duniani, ambavyo vimepewa jina la utani “viwanda vya kutengeneza digrii au stashahada”, yaani “degree mills”, ambavyo vinawadanganya Watanzania kwa kuwatunuku digrii za uzamivu za heshima.
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania inatambua madhumuni potofu ya ongezeko la vyuo hivyo bandia hapa nchini kwetu. Mantiki na matokeo ya digrii zitolewazo na vyuo hivyo batili kwa wanaotunukiwa na kwa jamii wanayoitumikia ni hatari na inawapunguzia heshima watunukiwa hao wao wenyewe na taifa zima kwa ujumla.

Kwa hiyo basi, Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania inatahadhalisha umma kuwa makini ili kuepuka wasitapeliwe na taasisi ambazo ni “viwanda vya kutengeneza digrii”, ambazo kwa hakika nia yao ni kujipatia pesa au kutafuta umaarufu kwa njia zisizo halali. Licha ya kutunuku digrii bandia za heshima, taasisi hizi pia zimewatapeli watu wengi pamoja na watanzania kwa kuwatunuku digrii, digrii za uzamili na hata za uzamivu (yaani doctorate degrees) bila ya wahusika kufanya kazi yoyote ya kitaaluma inayolingana na matakwa ya kutunukiwa digrii walizopewa, kwa kuwa tu waliweza kulipia gharama za digrii hizo.

Baadhi ya taasisi zinazotoa tuzo za digrii, na digrii za uzamivu za heshima zimefika mbali zaidi kwa kudai kuwa eti wanafanya hivyo kwa ajili ya kutoa heshima kwa Bara la Afrika kwa kuwa Waafrika walioleta mafanikio hawaheshimiwi na kuenziwa ipasavyo humu humu Barani Afrika, na kwa sababu hiyo pengo hilo linazibwa kwa kupewa tuzo ya digrii za uzamivu za heshima. Walengwa hasa ni watu maarufu na viongozi ikiwa ni pamoja na Marais na Mawaziri wa nchi zetu za Kiafrika, Wabunge, n.k.

Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania inaamini kuwa huu ni upotoshaji na kukwepa ukweli kwamba kwa hakika digrii nyingi za aina hii zinatolewa kwa misingi ya kubadilishana fedha au kutangaza umaarufu wa taasisi husika. Mfano wa taasisi za aina hii uliandikwa katika makala iliyotolewa hivi karibuni katika gazeti la “The Guardian” la hapa nchini la Jumatatu tarehe 19 Julai, 2010 ikihusisha taasisi moja ya kidini nchini Marekani. Imethibitika kuwa anwani ya mahali ilipo taasisi hiyo haiko bayana na taasisi hiyo haitambuliwi na nchi yoyote ya Kiafrika na hata nchini Marekani kwenyewe.

Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania inapenda kutahadhalisha umma kuhusu kuwepo kwa matukio haya na kutoa ushauri kwa yeyote anayehusika kuwasiliana na Tume kwa ajili ya ushauri na uthibitisho wa masuala yote yanayohusu elimu ya juu ili kuepuka kutumia gharama kubwa zisizo za lazima kupitia njia za mkato na hatimaye kutunukiwa “digrii ya kutengenezwa”, digrii isiyokuwa na thamani, iwe ya heshima au vinginevyo.

Prof. Mayunga H.H. Nkunya
KATIBU MTENDAJI
TUME YA VYUO VIKUU TANZANIA

Wednesday, August 4

KWA MTINDO HUU WANAFAIDIKA KWELI HAWA WAKULIMA ?


Kilimo Kwanza kinasisitiziwa sana kwa wakulima na hata kwa wafanyabiashara wa mazao mbalimbali,lakini je hawa wakulima halisia wanapewa /fikishiwa elimu thabiti juu uuzaji wa mazao yao,angalau basi wawe wanafaidika na kilimo chao badala ya kupata hasara ? Angalia pichani kama mkulima huyu anaeandaa bidhaa yake kwa ajili ya kuipeleka sokoni,je anafaidika kweli na jasho lake?

HOTUBA YA JANUARY MAKAMBA BAADA YA KUTANGAZWA KWA MATOKEO YA KURA ZA MAONI YA UBUNGE JIMBO LA BUMBULI KWA TIKETI YA CCM ILIYOTOLEWA KATIKA UKUMBI WA O


CCM Oyee! (Oyeee!)
CCM Oyee! (Oyeee!)
Bumbuli mpoo? (Tupoo!)


Nashukuru sana.

Sasa, nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa rehema zake. Tupo tumefika hapa leo tulipo kwasababu ameamua iwe hivyo. Ametujalia uhai, uzima na afya kati yetu. Kwahiyo ni muhimu kumshukuru.

Pili, napenda kuwashukuru wazazi wangu kwa malezi mazuri, kwa mchango wao mkubwa kwenye maisha yangu mpaka nimefikia hapa nilipofikia leo. Pia familia yangu – mke wangu na wanangu wawili – bahati mbaya hawapo [hapa] – wamesafiri. Lakini nawashukuru kwa kunitunza, kwa kukubali kukabiliana na hizi presha za siasa, na kuniunga mkono na kuwa na mimi wakati wote.

Lakini vile vile namshukuru bosi wangu, Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete. Namshukuru kwa kunikubalia nimtoroke kidogo kazi na kuja kufanya huu mradi, na namshukuru kwa ushauri na malezi ya kisiasa aliyokuwa akinipa wakati wote.

Lakini sana sana, nawashukuru wana-CCM wa Bumbuli kwa kuniamini - kwa kuniamini kwa kiasi kikubwa namna hii kwa kunipa kura nyingi sana. Waswahili wanasema, “Imani huzaa imani”. Imani waliyonipa kwa kura wanizonipa ni kubwa sana. Tutasherehekea leo, lakini kesho tutakumbuka kwamba kura hizo ni…maana yake ni kwamba wanategemea mengi kutoka kwangu. Na mimi naahidi kwamba sitawaangusha. Nitaibeba bendera ya Chama chetu cha Mapinduzi, na kuipeperusha na kuinadi Ilani yetu kwa uwezo wangu wote, kwa maarifa yangu yote na vipaji vyangu vyote nilivyojaliwa na Mwenyezi Mungu. Na naamini kabisa kwamba Chama chetu kitapata mshindi mkubwa sana kwenye jimbo la Bumbuli.

Lakini pia ningependa kuwashukuru wenzangu - wagombea wenzangu tulioshiriki nao, kwa kuonyesha ustaarabu mkubwa. Tumevumiliana, tumeheshimiana kwenye mchakato mzima. Ndugu yangu Kaniki mmemuona mwenyewe ni kijana mzuri, amekomaa vizuri.

Mzee Shelukindo – naomba niseme machache kuhusu Mzee Shelukindo, bahati mbaya hayupo hapa. Lakini kuvunjika kwa koleo sio mwisho wa uhunzi. Leo wana-CCM wameamua… jana wameamua, kwamba mwingine apeperushe bendera ya Chama chao kwenye uchaguzi mkuu. Lakini heshma ya Mzee Shelukindo katika nchi yetu bado ipo pale pale (makofi). Kwa kushindwa kura hizi za maoni, haina maana kwamba heshima yake na rekodi yake ya utumishi imepotea kabisa. Hapana. Ni maamuzi ya wanachama. Binafsi nitaendelea kumuheshimu kama Mzee, lakini [pia] kama kiongozi wa muda mrefu kwenye Serikali. Ni hazina kubwa ya uzoefu kwenye jimbo letu, na bado ni mwanachama wa CCM. Na binafsi nitaenda kumuomba rasmi…hatujakutana tangu tumalize mchakato huu, lakini nitamtembelea nyumbani kwake kumuomba kwamba tusaidiane kikazi (makofi).

Lakini naomba niwashukuru wapiganaji wangu walionisaidia kunadi jina langu. Walionisaidia kuwashawishi wana-CCM wa Bumbuli kwamba mimi nafaa. Nawashukuru kwa kazi nzuri. Ushindi huu uliopatikana ni matunda ya kazi yenu. Lakini vile vile naomba niwaambie kwamba uchaguzi umekwisha jana. Mpambano umekwisha. Sasa hivi sote tunarudi kwenye hema la Chama chetu cha Mapinduzi. Sina uadui na Mzee Shelukindo. Sina uadui na Bwana Kaniki. Sina uadui na Mzee Mshihiri (makofi). Sina uadui na mtu yoyote aliyeshiriki kwenye mchakato huu.

Kwahiyo wapiganaji wangu, nawaomba sana sana sana tuache tambo. Tuache kutambiana. Uchaguzi umekwisha jana. Kazi ya kunipigania imeisha, tunaanza kazi ya kukipigania Chama chetu. Ndio kazi iliyo mbele yetu, na naomba tuifanye kwa umoja, tukishirikiana na wale ambao hawakuniunga mkono kwenye mchakato huu. Kwa nguvu ile ile ambayo mlinipigania mimi, naomba sasa nguvu hiyo muielekeze katika kukipigania Chama chetu kwenye uchaguzi mkuu wa mwezi Oktoba mwaka huu.

Naomba vile vile nitoe shukrani na pongezi zangu kwa uongozi wa Chama Wilaya, Katibu wa Wilaya na timu yake. Wilaya yetu ina majimbo matatu na kata 44. Zoezi hili ni zoezi kubwa, hasa kusimamia chaguzi za madiwani katika kata zote hizi. Ni kazi inayohitaji uwezo mkubwa, inahitaji rasilimani za uendeshaji na uwezo mkubwa wa kiutawala. Natambua kwamba zimejitokeza kasoro za hapa na pale, lakini naamini kwamba kasoro hizo zinatokana na upya wa mfumo wetu huu mzuri wa kurudisha demokrasia kwa wanachama kuchagua ni nani wawasimamishe kupeperusha bendera ya Chama kwenye uchaguzi wa wabunge na madiwani. Naamini kwamba matatizo yaliyojitokeza yatashughulikwa, na wakati ujao tutakuwa na utaratibu mzuri zaidi. Lakini vile vile naamini zaidi kwamba kasoro zilizojitokeza hazikumnyima mtu haki, na kwamba matokeo haya ya Bumbuli ni kielelezo halisi cha matakwa ya wanachama wa CCM wa Jimbo la Bumbuli.

Na mwisho, napenda kuwashukuru wote waliojitokeza hapa kunisikiliza, na nawatakia jioni njema. Nashukuru sana. (makofi)

January Makamba,
Agosti 2, 2010.

Monday, August 2

the most popular woman on the web

# 50 Eva Langoria

7,360,000 Results


divider-grey2

#49 Scarlett Johansson

7,500,000 Results


divider-grey2

#48 Carmen Electra

7,620,000 Results

divider-grey2

#47 Tina Fey

7,910,000 Results

divider-grey2

#46 Adriana Lima

7,930,000 Results

divider-grey2

#45 Lily Allen

9,200,000 Results

divider-grey2

#44 Sarah Jessica Parker

9,470,000 Results

divider-grey2

#43 Kelly Clarkson

9,690,000 Results

divider-grey2

#42 Carrie Underwood

9,740,000 Results

divider-grey2

#41 Amy Winehouse

10,000,000 Results

divider-grey2

#40 Vanessa Hudgens

10,100,000 Results

divider-grey2

#39 Katie Price

10,200,000 Results

divider-grey2

#38 Ashley Tisdale

10,700,000 Results

divider-grey2

#37 Hilary Duff

11,700,000 Results

divider-grey2

#36 Marilyn Monroe

11,800,000 Results

divider-grey2

#35 Heidi Montag

12,200,000 Results

divider-grey2

#34 Demi Mooree

12,700,000 Results

divider-grey2

#33 Jennifer Aniston

13,300,000 Results

divider-grey2

#32 Hilary Clinton

13,800,000 Results

divider-grey2

#31 Ciara

14,300,000 Results

#30 Kristen Stewart

14,400,000 Results

divider-grey2

#29 Betty White

14,500,000 Results

divider-grey2

#28 Pamela Anderson

15,200,000 Results

divider-grey2

#27 Fergie

15,600,000 Results

divider-grey2

#26 Jessica Alba

16,400,000 Results

divider-grey2

#25 Christina Aguilera

16,900,000 Results

divider-grey2

#24 Sandra Bullock

18,400,000 Results

divider-grey2

#23 Kim Kardashian

19,700,000 Results

divider-grey2

#22 Katy Perry

19,900,000 Results

divider-grey2

#21 Michelle Obama

19,100,000 Results

#20 Lindsay Lohan

20,100,000

divider-grey2

#19 Jessica Simpson

20,900,000

divider-grey2

#18 Sarah Palin

21,000,000

divider-grey2

#17 Mariah Carey

22,200,000

divider-grey2

#16 Jennifer Lopez

24,200,000 Results

divider-grey2

#15 Megan Fox

24,200,000 Results

divider-grey2

#14 Oprah

24,300,000 Results

divider-grey2

#13 Angelina Jolie

28,500,000 Results

divider-grey2

#12 Taylor Swift

28,600,000 Results

divider-grey2

#11 Shakira

28,700,000 Results

#10 Avril Lavigne

28,900,000 Results

divider-grey2

#9 Paris Hilton

33,200,000 Results

divider-grey2

#8 Miley Cyrus

34,100,000 Results

divider-grey2

#7 Princess Diana

42,200,000 Results

divider-grey2

#6 Britney Spears

46,600,000 Results

divider-grey2

#5 Rihanna

53,900,000 Results

divider-grey2

#4 Beyonce

55,200,000

divider-grey2

#3 Madonna

61,300,00 Results

divider-grey2

#2 Kesha

76,100,000 Results

divider-grey2

#1 Lady Gaga

85,900,000 Results